Skip to main content

TIGO GAWIO

 TIGO NI KAMPUNI YA KWANZA DUNIANI KUGAWA FAIDA KWA WATEJA WAKE. Gawio ni huduma ya tigo inayompatia mteja wetu faida ya matumizi yake ya tigo pesa kwa kila miezi mi tatu.




     Meneja Mkuu wa Tigo Diego Gutierrez akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) mapema leo kuhusu kutoa gawio la kiasi cha shilingi bilioni 14.25 lililolimbikizwa kwenye akaunti ya mfuko wa fedha wa Tigo Pesa kwa ajili ya wateja wao. Kulia ni Mkuu wa Idara ya Tigo Pesa Andrew Hodgson na Meneja Masoko na Usambazaji wa Tigo Pesa Catherine Rutenge (kulia).


   

Mkuu wa Idara ya Tigo Pesa Andrew Hodgson akijibu maswali ya waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu gawio la shilingi bilioni 14.25 litakalo anza kutolewa kwa wateja wa kampuni hiyo. Gawio hili litawanufaisha jumla ya watumiaji milioni 3.5 wa Tigo Pesa nchini. Kushoto ni Meneja Mkuu wa Tigo Diego Gutierrez.



Tigo Tanzania leo imetangaza itatoa gawio la kiasi cha shilingi bilioni 14.25 (sawia na dola za kimarekani bilioni 8.7) lililolimbikizwa kwenye akaunti yake ya mfuko wa fedha wa Tigo Pesa kwa ajili ya wateja wake. Hii inaifanya kampuni hiyo kuwa mtandao wa simu ya kwanza duniani kutoa gawio la fedha kutokana na huduma ya kutuma na kutoa fedha.
Akaunti ya mfuko wa fedha wa Tigo Pesa (Tigo Pesa Trust Account) ni akaunti ambayo fedha zote za Tigo Pesa zinakusanywa na kuhifadhiwa toka huduma ya Tigo Pesa ilipoanza miaka mine iliyopita. Kwa sasa Tigo ipo tayari kutoa gawio la fedha hizo ambazo zilikuwa zinazaa faida baada ya kuridhiwa na  Benki Kuu ya Tanazania (BOT) kwa barua rasmi ya kutokuwa na pingamizi iliyopokelewa Julai mwaka huu.
Meneja Mkuu wa Tigo Diego Gutierrez amesema kwamba gawio hilo la faida itawanufaisha wateja wote wa Tigo, wakiwemo mawakala wakuu, mawakala wa reja reja na mteja mmoja mmoja, mtumiaji wa Tigo Pesa.
“Kwa miaka mitatu na nusu sasa mfuko wa fedha wa Tigo Pesa ulikuwa ukikusanya faida kwa kiwango cha asilimia 5 hadi 12, na mpaka Juni mwaka huu faida hiyo imefikia shilingi bilioni 14.25. Lengo ni kuwapatia wadau wetu wa Tigo Pesa fursa ya kupata faida kutokana na kiasi cha fedha walichoweza kukiweka katika akaunti zao za Tigo Pesa,” alisema Gutierrez.
Aliongeza, “Wastani ya faida ambayo mteja yeyote ataweza kupata inatofautiana na wastani wa fedha ambayo ataweza kubaki nayo kwenye akaunti yake ya Tigo Pesa kwa siku. Kwa hivyo viwango vya faida vitatofautiana kati ya wakala mkuu, wakala wa reja reja au mteja wa kawaida.”
Gawio hili litawanufaisha jumla ya watumiaji milioni 3.5 wa Tigo Pesa nchini, wakiwemo mawakala wakuu na mawakala wa reja reja ambao wana umuhimu wa kipekee kwenye muundo mzima wa mtandao wa huduma ya kutuma na kupokea pesa nchini Tanzania. 
“Ukiondoa kiasi cha dola milioni 100 za kimarekani ambazo tulikuwa tumeahidi kuendelea kuwekeza nchini kila mwaka kama mpango moja wapo wa kuongeza ufanisi katika mtandao wetu, gawio la mfuko wa fedha wa Tigo Pesa ni uwekezaji wa moja kwa moja kwa maisha ya Watanzania, kwa sababu itasaidia kuinua kiwango cha kipato na hali za kiuchumi kwa wateja wetu. Pia ni udhibitisho kwamba kampuni yetu inaendelea kuwajibika katika kuwajumuisha wananchi katika mzunguko wa fedha na kiuchumi kwa kupanua wigo wa matumizi ya Tigo Pesa kote nchini,” alisema Gutierrez

Comments

Popular posts from this blog

TIGO HAND SET CONFIGURATION - KUUNGANISHA INTERNANT KWENYE SIMU

Kuunganisha internet kwenye sim inategemea na simu yenyewe,ni aina gani na mfumo wake ni upi? ->>kina aina nyingi za simu lakini baadhi unaweza kuzigawa katika makundi ma nne (4) 1. SMART PHONE 2. BLACK BERRY 3. IPHONE ( IPOD ) 4. NORMAL               1. ANDROID Simu za android unaweza kuziweka katika makundi mawili kutegemea na SETTING ZAKE -Tofauti ya hizi ni maneno WIRELESS and NETWORK na MORE NETWORK. >>JINSI YA KUSETI ANDROID (Njia ya kwanza ) Bonyeza MENU Nenda kwenye SETTING Kisha ingia WIRELESS AND NETWORK  Kisha ingia MOBILE NETWORK Nenda  ACCESS POINT NAME ( APN ) Nenda ADD NEW    Name andika TIGOWEB APN andika  TIGOWEB Authentication type weka  CHAP SAVE NJI YA PILI Bonyeza MENU Nenda kwenye SETTING Kisha ingia kwenye MORE SETTING Halafu nenda (MOBILE NETWORKS  Nenda ACCESS POINT NAME (APN) Nenda kwenye ADD   Name andika ( TIGOWEB ) APN ...

TIGO SHOP / NAMBA YA MAAJABU / NAMBA YA VIFURUSHI

ULIPO TUPO TIGO SHOP / NAMBA YA MAAJABU / NAMBA YA KUJIUNGA VIFURUSHI   TIGO SHOP / NAMBA YA MAAJABU / NAMBA YA KUJIUNGA  >>Tigo shop Menu *148*00#    -Ni namba ambayo inakupa mteja vifurushi mbalimbali vya kutuma SMS ,INTERNET, Pamoja na sms. ->itakupa vifurushi vifuatavyo ->>OFA Maalum (kifureshi namba moja) -Internet BURE     ,Kifurushi hiki kitakupa bure MB 100 Bilakikomo cha spidi kutumia kati ya saa 12 ASUBUHI mpaka   saa   2 ASUBUHI: BILA KULIPIA -MIA MIA Bilakikomo     Ndugu mteja utaongea bila kikomo TIGO -TIGO Na utalipia sh 100 kwa kila simu uipigayo,KUJIUNGA NI BURE -USIKU Bilakikomo (GB 30 ) =Sh 1,000   kifurushi hiki kinakupa GB 30 Bila kikomo cha spidi,mteja Utatumia kati ya saa 5 usiku Hadi sdaa 11 Asubuhi Na kitadumu kwa muda wa siku 2 MFULULIZO Kwa shilingi 1,000 tu.  - 999 sh = 900 min + 500 SMS      Ki...